Maabara ya Akiolojia ya Pleistocene (PAL)
Maabara ya Akiolojia ya Pleistocene (PAL) ni kituo kipya cha utafiti katika Taasisi ya Historia- CSIC (Baraza la Kitaifa la Utafiti la Uhispania), lililoko Centro de Ciencias Humanas y Sociales, CCHS, Madrid. Maabara hii inalenga kukuza utafiti juu ya akiolojia ya mageuzi ya binadamu, zana za kale za mawe na utafiti wa jamii za wawindaji katika kipindi cha Pleistocene.
PAL inajuhusisha na tafiti za kiakiolojia hasa tafiti juu ya asili ya teknolojia. Utafiti huu unajumuisha uchimbaji wa kiakiolojia nchini Afrika ya Mashariki na Uhispania, tafiti za zana za mawe zinazofanyika PAL zinahusisha utafiti wa teknolojia ya mawe, majaribio ya kunakili na alama za matumizi.
